Job 14


1 a“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke
siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.

2 bHuchanua kama ua kisha hunyauka;
huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.

3 cJe, unamwekea jicho lako mtu kama huyo?
Je, utamleta mbele yako katika hukumu?

4 dNi nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi?
Hakuna awezaye!

5 eSiku za mwanadamu zimewekewa mpaka;
umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake
na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.

6 fHivyo angalia mbali umwache,
hadi awe amekamilisha muda wake
kama mtu aliyeajiriwa.


7 g“Kwa maana lipo tumaini kwa mti;
kama ukikatwa utachipuka tena,
nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.

8 hMizizi yake yaweza kuchakaa ardhini
na kisiki chake kufa udongoni,

9 ilakini kwa kupata dalili ya maji utachipua
na kutoa machipukizi kama mche.

10 jLakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake;
hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!

11 kKama vile maji yatowekavyo katika bahari,
au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,

12 lndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke;
hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena,
wanadamu hawataamka au kuamshwa
kutoka kwenye usingizi wao.


13 m“Laiti kama ungenificha kaburini,
Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

na kunisitiri hadi hasira yako ipite!
Laiti ungeniwekea wakati,
na kisha ukanikumbuka!

14 oJe, kama mtu akifa, aweza kuishi tena?
Siku zote za kazi zangu ngumu
nitangojea kufanywa upya kwangu.

15 pUtaniita nami nitakuitika;
utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.

16 qHakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu,
lakini hutazifuatia dhambi zangu.

17 rMakosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko,
nawe utazifunika dhambi zangu.


18 s“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika
na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,

19 tkama maji yamalizavyo mawe,
na mafuriko yachukuavyo udongo,
ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.

20 uHumshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka;
waibadilisha sura yake na kumwondoa.

21 vKama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu;
kama wakidharauliwa, yeye haoni.

22 wYeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe,
naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
Copyright information for SwhKC